ROZARI TAKATIFU NA ROZARI HAI
ROZARI HAI
(a)Historia
Karne ya 18 LionsUfaransa.
Paulina alitekwa na
wazo namna ya kuwashawishi watu kupenda kusali Rozari ambayo imekuwa ikisaliwa
na wazee na wacha Mungu wachache. Ibada
ya Rozari ilielekea kuwa imepitwa na
wakati katika maisha ya wengi. Kulikuwa
na watu wachache waliokuwa wakijitahidi katika ibada hii lakini mshikamano wao
haukuwa wa uhakika kutokana na wimbi la wakati huo kuwa starehe iliwekwa mbele.
Paulina alielewa ibada binafsi za watu hao wa pekee ni kama “cheche
bila kuhusisha wengi katikati ya giza nene.”
Kinachohitajika katika giza nene
siyo cheche bali mwanga; “Mwanga unaoishi au Mwanga wa kudumu”
LINAFANYIKAJE HILO?
Tunakusanya cheche mpaka kuzifanya mwanga unaoishi.
(ROZARI HAI
)-Mwanga uliounganika
unaoishi na kuwaka katika upendo na kwa
upendo.
Kupitia sala zake Paulina - Mungu alimwonyesha Paulina njia-RAHISI SANA”
KUGAWA ROZARI KATIKA VIPANDE
15 kwa sasa 20 SAWA NA MAFUMBO 15 kwa sasa 20 YA ROZARI TAKATIFU.
Kwa jinsi kwamba kila
mtu atasali kumi moja tu na kutafakari
fumbo husika la kumi hiloROZARI HAI- Hii siyo ibada ya mtu binafsi ni sala ya familia, familia
inayoasali kila siku. Mt 18:19 -20 mdo 1:14
Mwenye heri Paulina
alianzisha Rozari Hai 1826
Ilitambuliwa rasmi na kujazwa
Rehema nyingi na Papa Gregory 16 na kuwekwa katika
kitabu cha sheria za kanisa tarehe 27/1/1832
Rejea-
“Faraja ya uponyaji wa Moyo wa Maria uk
3 sura ya 3, ya 4 na ya 5.
(b)Rozari Takatifu na Rozari Hai.
Wazo la kupata ufafanuzi kuhusu tofauti kati
ya Rozari Takatifu na Rozari Hai ni zuri na la msingi. Kimsingi hakuna
tofauti kati ya Rozari na Rozari Hai.Ni Rozari ile ile ya Mama yetu, ambayo imezoeleka katika Kanisa
Katoliki, ikisaliwa na mtu binafsi au jumuiya.
Sasa katika Rozari Hai, ni Rozari ile ile
inayosaliwa lakini sasa kama chama
cha kitume kijulikanacho kama ROZARI HAI.
Kama chama cha kitume, Rozari Hai inalenga
kimsingi kusali Rozari kama FAMILIA YA
KIROHO. Kwa mantiki kwamba, ingawa wana Rozari Hai, kimwili wametawanyika
katika sehemu mbalimbali ulimwenguni, kwa majitoleo yao binafsi katika sala
wanakuwa pamoja kama familia ya kiroho.
Kwa majitoleo binafsi katika kusali Rozari
muhusika anaweza kusali kwa nia yake maalum lakini katika Rozari Hai, tunasali
kwa nia kuu mbili:
1. Ushindi wa Moyo Imakulata wa Maria.
2. Kwa heshima ya Mt. Filomena.
Hivyo hizi nia za msingi pamoja na upendo
wetu katika kuwajali wengine katika shida zao, tunaunganika pamoja kama familia
moja inayomwelekea Mama Maria,
chini ya usimamizi wa Mt. Filomena.
Wanachama wa Rozari Hai, wana wajibu
wa kusali kwa tafakari fungu moja tu la Rozari kila siku. Kwa kuwa ni
jumuiya au familia iliyounganika katika nia na matendo ya huruma, sala ya kila
mmoja inakuwa sala ya wote. Hii ina maana kwamba kila mwanachama, kiroho
anasali mamilioni au mabilioni ya mafungu kila siku na kushiriki kikamilifu
zawadi zote za kiroho zitokanazo na sala hizo.
NAMNA
YA KUSALI:
1.
Kila
Mwanachama atapewa fungu moja la Rozari la kusali kila siku
2.
Kila
Mwanachama atapewa fumbo la kutafakari kila asalipo Rozari (fungu lake).
3.
Akumbuke
kutolea nia za msingi zilizotajwa hapo juu.
MFANO: Mimi binafsi naweza
kupiga magoti chumbani mwangu nikasali mafungu yote ishirini ya Rozari. Ni mimi
peke yangu nasali yale mafungu ishirini, kwa nia zangu binafsi na hatimaye
nitapata mastahili ya mafungu ishirini tu. Sasa, katika Rozari hai, kila mwanachama
anayesali fungu moja ni kama anasali mamilioni ya mafungu kwa sababu wanachama
wote wameunganika kuwa kitu kimoja (mmoja) kiroho, katika Moyo Imakulatawa Maria
wakisali popote walipo kwa:
-
Sauti moja
-
Akili moja
-
Moyo mmoja
-
Nia moja
-
Kama familia moja
Kwa hiyo, mambo hayo makuu matano, ndiyo kwa
kiasi Fulani yanatofautisha kati ya Rozari Hai na ile ya kawaida.
Hivyo, Rozari Hai ni namna ya kusali Rozari yenye nguvu sana
na faida zaidi.
Ndiyo maana Papa Gregori wa 16 na
wengine waliofuatia baada yake hawakusita kuipitisha kwa ajili ya kanisa zima.
Ukweli ni kwamba majitoleo ya roho moja
moja zilizotengana ni kama cheche ya moto katikati ya giza nene, ambayo huwaka
bila kutoa ndimi za moto. Lakini kwa njia ya umoja wetu wa upendo katika kusali
Rozari Hai,hizi cheche
zinaunganika pamoja na kuwa moto uwakao daima bila kuzimika. Ndiyo maana
tunaita Rozari Hai kwa sababu ni moto unaowaka ukitoa mwanga tofauti na cheche
ya moto ya mtu mmoja mmoja: kwa Kiswahili tunasema UMOJA NI NGUVU. Na kwa kuwa wanachama
wake wote wameunganika kwa ujumla katika hii Rozari Hai kokote walioko basi kwa
ujumla tunaiita CHAMA CHA UTUME WA
ROZARI HAI YA MT. FILOMENA MAHALI POTE.
Kila Mwanachama wa Rozari Hai ni Mmisionari,
kwa kuwa anasali kwa ajili ya wokovu wa ulimwengu. Hii ndiyo maana
ya USHINDI WA MOYO IMAKULATA WA MARIA.
Na ndiyo hasa Yesu alimaanisha katika sala yetu ya Baba yetu: UFALME WAKO UFIKE, UTAKALO LIFANYIKE DUNIANI KAMA MBINGUNI. Kila Mkristu Mkatoliki
anayehusudu wokovu wa Dunia, anayelipenda kanisa, Mama yetu Bikira Maria, na
anayeamini nguvu ya Rozari, si rahisi kukataa kujiunga na Rozari Hai. Hivyo
basi uanachama uko wazi kwa wote bila kujali umri: Hakuna mipaka katika idadi,
kwani hadi sasa idadi inafikia zaidi ya wanachama milioni kumi na sita
ulimwenguni. Kati yao wakiwemo maelfu ya Mapadre, Masista na idadi nzuri ya
Maaskofu. Askofu Telesphore Mkude ni Askofu wa kwanza Tanzania kuwa Mwanachama
wa Rozari Hai.
Wanachama wote wanaandikishwa rasmi na
kupewa kadi ya fungu la kusali. Ni matarajio yetu kwamba maelezo haya yatawatia
moyo kuitangaza Rozari Hai kama habari njema katika sehemu zenu.
Wanachama wa Rozari Hai hawahitaji kukusanyika ili kusali
mafungu yao. Mtu anaweza kusali wakati wowote mahali popote, usiku au
mchana – ili mradi asali fungu lake kadri atakavyoona inafaa.
Hata hivyo, kama chama cha Rozari na mfano
wa familia, wanachama katika kila Parokia au Kigango wanapaswa kukutana walau mara
moja kwa mwezi Kanisani ili
kutiana nguvu na moyo wa kusali mafungu yao, na pia kutumia muda huo kutia uhai
katika utume mbalimbali walionao. Na hapa inapendekezwa wakutane Jumapili
ya tatu ya kila mwezi.
Utume
mbalimbali tulionao katika Rozari Hai ni:
Wanachama kusali kila siku fungu la Rozari walilopewa,
wakitafakari juu ya fumbo husika walilopewa kila mmoja.(Hili ni la msingi)
Halafu
kuna;
1.
Kutembelea
wagonjwa nyumbani na hospitalini.
2.
Kuwasaidia
wale wanaohitaji msaada wa kiutu.
3.
Kuhimiza
majitoleo kwa Mama yetu kwa kufanya semina na mikutano.
Kwa hiyo kuna utaratibu kwamba katika kila
sehemu ambako tuna wanachama, kunapaswa kuwa na watu kati ya watano (5) na saba
(7) kama viongozi, wakishirikiana na wanachama. Ambao ni; Mwenyekiti, Makamo
Mwenyekiti, Katibu, Makamo katibu, Mhazini, Mkutubi na Mratibu.
Hapa chini ni utaratibu wa sala wa kila
mwezi wa kusali katika kusanyiko la wana Rozari Hai:
1. Kwa
jina la Baba ………………………………
2. Uje
Roho Mtakatifu (au wimbo wa Roho Mtakatifu)
3. Rozari
ya makumi matano
4. Litania
ya Bikira Maria
5. Wimbo
wa Bikira Maria
6. Tasbihi
/ Taji dogo la Mt. Filomena
7. Litania
ya Mt. Filomena
8. Wimbo
wa Mt. Filomena
9. Sala
za Mt. Filomena
10. Mazungumzo ya kiroho (dakika 5 – 10)
11. Sala za kukua kwa Rozari Hai katika Parokia,
Jimbo na Taifa.
-
Baba yetu x 1
-
Salaam Maria x 3
-
Atukuzwe Baba x 1
12. Sadaka
13. Mazungumzo,
taarifa, kugawa wajibu mpya, nk.
14. Matangazo
15. Sala za kufunga
·
Kuwaombea wagonjwa na wenye shida mbalimbali
-
Baba yetu x 1
-
Salaam Maria x 1
-
Atukuzwe Baba x 1
-
Salaam Malkia
Licha ya mikutano ya sala, huwa tunafanya NOVENA kabla ya sikukuu au sherehe za
Bikira Maria kama: Jan. 10, Machi 25, Mei 13, Julai 16, Agosti 11 na 15,
Oktoba 7
na Disemba 8.
(c)Namna ya kusali kumi lako.
Sala
Tuungane na wanachama wa Jumuiya ya
Rozari Hai Duniani kote na kutolea fungu hili la Rozari Takatifu
kwa; Ushindi wa Moyo Imakulata wa Maria,
kwa heshima ya Mt. Filomena, Paulina
Jaricot,na Mt.Theresia ; Kwa ajili ya Maaskofu wote,
Mapadre na Watawa, wanachama, wagonjwa na wanaoteseka; watakaokufa leo ili wapewe neema ya uvumilivu
na hatimaye kifo chema , pia kwa ajili ya amani katika familia zetu.
………………KUMI LANGU…………………….…
(hapa Sali
kumi lako)
Kumi
linajumuisha; Fumbo husika, Baba yetu
x 1, Salamu Maria x 10
-zikiambatana na tafakari ya fumbo husika, Atukuzwe Baba x 1
na Ee Yesu mwema……. .
…………………………………………………………………….
(Kisha endelea na sala hii )
Ee Maria
uliyeumbwa pasipo dhambi ya asili, tunaomba kwako upendo mkamilifu kwa Yesu
Kristu !
Ee Roho
Mtakatifu nakutolea Moyo wa Kiekaristi
wa Yesu, Damu yake Takatifu; Moyo
Imakulata wa Maria wenye uchungu, mpole,
mnyenyekevu na mtii, kulipia makosa yangu yote na madharau yangu. Najitolea
kabisa kwako. Naweka matumaini yangu yote kwako. Amina.
Tafakari
----Rejea kijitabu “FARAJA YA UPONYAJI WA MOYO WA MARIA Uk.8
(a) Rehema kwa wanachama wa Rozari
Hai.
Kwa kusali Rozari hai
tunaweza kujipatia rehema nyingi sana, ambazo tunaweza kuzitolea kwa ajili ya
roho za Toharani. Nazo ni kama zifuatazo.
1.
Rehema kamili
siku ya kupokelewa katika ushirikawa
Rozari hai.
2.
Rehema kamili
kila jumapili ya tatu ya kila mwezi na pia siku za sikukuu ya Yesu na Bikira
Maria.
3.
Rehema kamili
siku za sikukuu zifuatazo: Epifania,
Ekaristi, Utatu Mtakatifu, Watakatifu Petri na Paulo na sikukuu ya Bikira Maria
wa mlima Karmeli.
4.
Rehema kamili saa ya kufa.
5.
Rehema zote
zilizotolewa kwa wenye kusali Rozari nzima (Tasbihi nne).
6.
Rehema nyingine nyingi
sana, ambavyo ni vigumu kuziorodhesha hapa zote.
-Rejea kijitabu-“ Faraja ya
Uponyaji wa Moyo wa Maria” Uk6 sura ya 8
Nitapataje kitabu cha Rozari hai
ReplyDelete