ROZARI TAKATIFU
Historia
Rozari ni taji
la Mawaridi.Ni neno la kilatini lenye maana ya Bustani ya maua ya waridi.
Rozari
inahusishwa na Zaburi 150 ambazo Wayahudi walizitumia kama sala hekaluni.
Karne ya 12
walizuka wazushi wapinga dini, walioitwa Waalbigensia. Hawa walienea Kusini ya
Ufaransa na Kaskazini ya Italia.
Baba Mtakatifu
wa wakati huo alimteua Padre Dominiki awahubirie. Aliwahubiria kwa maarifa yake yote lakini
walizidi kushupaa na kumdhihaki. Mt.Dominiki alipoona kuwa uzito mkubwa wa
dhambi walizotenda watu unazorotesha kuwageuza Waalbigensia, alikwenda msitu wa
Toulouse na kusali mfululizo kwa siku tatu usiku na mchana. Akiwa msituni alijitesa vikali ili kuomba
huruma ya Mwenyezi Mungu.
Alijitesa kiasi kwamba
alijipiga mijeledi mwishowe alizirai kabisa. Mama yetu alimtokea akiwa na
Malaika watatu na kumwambia: “Mpendwa Dominiki, je, unajua Utatu
Mtakatifu unataka kutumia chombo gani kuurekebisha ulimwengu? ’’ Mt.
Dominiki alijibu: “ Wewe unaelewa zaidi kuliko mimi maana wewe uko karibu zaidi na Mwanao
Yesu Kristu na umekuwa nyenzo kuu ya wokovu wetu”. Bikira Maria
alimjibu: “Nataka ujue kuwa katika vita kama hivi ukitaka kuvishinda, hubiri
Rozari yangu; ukitaka kuishinda mioyo migumu na kuirejesha kwa Mungu, hubiri
Rozari yangu.’’
Baada ya Dominiki kuihubiri
Rozari na kusali Rozari, wazushi zaidi ya laki moja waliongoka.(Rejea: Siri ya
Rozari, uk.24-26)
Toka hapo sala ya Rozari ilipata kuenea
upesi sana popote Duniani, na waumini kuisali sala hiyo kwa bidii na juhudi
kubwa sana.
Sala ya Rozari Takatifu inahitaji unyenyekevu
mkubwa. Katika kusali Rozari unarudiarudia mambo unayoyajua na kuyafahamu.
Wenye majivuno wanaidharau, lakini wanaompenda Bikira Maria na Mungu
wanaithamini sana. “Ni nani kama Mungu wetu aliyekaa juu na anawaangalia walio
chini, mbinguni na duniani?”(Zaburi
113;5-6)
Sala ya
Rozari ni mwigo wa wimbo wa Malaika wakuu wanaosimama mbele ya kiti cha enzi
cha Mungu wakiimba kwa kupokezana: Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu, Bwana Mungu
wa majeshi, mbingu na nchi zimejaa utukufu wako. Siri hii ya kiti cha enzi cha
Mungu imefunuliwa (Isaya 6:3). Vivyo hivyo wenye kusali sala ya Rozari Takatifu ya
familia au ya jumuiya wanapokezana kumsifu Mama Bikira Maria.
Je, si vema na sisi pia kumtukuza Mama wa Mungu vile kama hao Malaika wakuu?
Ameshuhudia mwenyewe jinsi anavyoipenda sala hii alipomtokea Mtakatifu Bernadetta Soubiru huko
Lourdes, Ufaransa ya Kusini tarehe 11/2/1858 mpaka 16/7/1858. Alikuwa ameshika
Rozari mikononi mwake. Akasali pamoja na huyo binti mpendevu wake.
Alitabasamu wakati huyo binti alipomsalimia kwa ‘Salamu Maria’. Alimtukuza mwanaye hapo
sala ya ‘Baba yetu’ iliposemwa;
lakini alijiunga na Bernadeta kusali ‘Atukuzwe
Baba’.
Nov. 1877, Papa Pius wa tisa alisema: “Nawahimiza
msali sala ya Rozari Takatifu kwa sababu ni Mama wa Mungu mwenyewe
aliyetufundisha jinsi ya kuisali”.
Mwenyeheri Alan anasema: “Sala ya Rozari Takatifu ni hazina
kubwa ya Neema; na wakosefu wengi wamepata wokovu kwa njia yake. Ni njia ya
ajabu madhubuti ya kubatili dhambi na kujipatia neema”. Baba Mtakatifu Gregori wa XIV alisema: “Sala
hii inaongeza fadhila za watu wema.”
Naye Baba Mtakatifu Leo wa XIII aliongeza:
“Ni jambo la ajabu sana kwamba watakatifu
wote walioishi baada ya sala hiyo kufundishwa na Mtakatifu Dominika; waliisali
sala hiyo kwa uaminifu mkubwa, Nayo ikawajalia nguvu kubwa ya kujitakasa”.
Mtakatifu
Fransisko wa Sale na Mtakatifu Alfonsi wa Ligori waliweka nadhiri ya kusali
sala ya Rozari Takatifu kila siku kwa ibada kubwa.
Baba Mtakatifu Pius wa V na Mtakatifu Karoli Boromeo
ingawa walikuwa na shughuli na kazi nyingi kila siku, hawakuacha kuisali kila
siku; isitoshe waliisali katika jumuia pamoja na wenzao.
Mtakatifu Karoli Boromeo, aliwataka na kuwalazimisha
wanafunzi wa seminari kuisali sala ya Rozari Takatifu kila siku. Mwenyeheri
Klementi Hofbaure aliisali kila siku na kila mara alipokuwa faraghani, haswa
alipokuwa akipita katika mitaa ya mji wa Vienna aende kuwahudumia wagonjwa.
Sala hiyo ilimpatia waongofu wengi. Alizoea kusema: “Kila mara niliposali sala ya
Rozari Takatifu kuomba wokovu wa watu wenye dhambi, sala yangu ilisikilizwa”
Kuna watu waliita sala ya Rozari Takatifu kuwa ni “Kipimo cha hali ya Ukristu”
(“Thermometer of Christianity”) kwa
kweli hawakukosea. Tazama! Pale iliposaliwa
kwa ibada na uaminifu mkubwa, utaona matokeo
na matunda mazuri ya maisha ya Kikristu. Imani inasitawi na kutawala. Pale inapodharauliwa, unaweza
kubashiri uchakavu na kupooza kwa maisha ya Kikristu. Mazoea ya kusali sala ya
Rozari ndiyo sababu pekee inayodumisha hazina ya imani kwa karne nyingi.
Nyakati za maafa makubwa, waumini, kwa kusali sala
ya Rozari Takatifu, waliweza kupata misaada ya ajabu na wakati mwingine
miujiza. Ushindi wa vita vya Lepanto, mwaka 1571, usingalipatikana kama watu wasingesali
sala hiyo ya Rozari. Ushindi wa Belgrade, mwaka 1716, nao
ulipatikana kwa kusali Rozari. Yasemekana vema kwamba, maadui walipigwa zaidi
kwa punje au shanga za Rozari kuliko kwa risasi za maaskari. Baba Mtakatifu Gregori wa XIII
alifahamu jinsi ushindi huo ulivyopatikana kwa njia ya kusali Rozari Takatifu.
Akaamuru sikukuu ya Rozari Takatifu
iadhimishwe tarehe 7 ya mwezi Oktoba.
Baba Mtakatifu Sixtus IV alisema “Sala
ya Rozari iliuepusha ulimwengu na majanga makubwa yaliyokuwa yakiuogofya;
ilituliza hasira ya Mungu.”
Baba Mtakatifu Gregori wa XIII naye alisema wakati
Mtakatifu Dominiki alipotumia sala ya Rozari ilikomesha maovu ya nyakati hizo,
na kwamba sala hiyo ina uwezo wa Kimungu.
Baba Mtakatifu Leo XIII, tarehe 1/9/1883, alitilia
mkazo mkubwa uwezo na uhakika wa sala ya Rozari kutokana na kushinda maovu ya
nyakati zake. Naye Baba Mtakatifu Pius wa IX alirudia kusema: “Wanangu nisaidieni kushinda maovu ya
kanisa na ya jumuiya, si kwa upanga, bali kwa sala ya Rozari Takatifu.”
Nguvu za sala hiyo zaweza kujulikana na tu kwa ibada kubwa. Hakuna sala
nyingine yeyote inayoweza kumtuliza mtu katika majonzi na dhiki au inayoweza
kuondoa mahangaiko na fadhaa kuliko sala ya Rozari Takatifu. Sala ya Rozari
ambayo inaitwa “Injili ndogo” inampa
mtu anayeisali vema na kwa juhudi kubwa amani inayoahidiwa katika Injili.
Baba Mtakatifu Leo wa XIII aliamuru kuutolea kwa miaka yote mwezi
wa Oktoba uwe mwezi wa Rozari Takatifu.
Naye Baba Mtakatifu Pius wa IX aliacha kama wosia wake kwa waumini wote: “Salini
pamoja kila jioni katika familia zenu sala ya Rozari Takatifu: Sala hii ni
nyepesi na nzuri, iliyo na wingi wa Rehema, ni
wosia wangu wa mwisho ninaowaachieni”. Siku moja pia
aliwaonyesha waumini Rozari yake akisema: “Hii ndiyo Hazina kubwa ya Vatica.” Ingekuwa jambo la maana sana na la
kufaa kama kila mmoja wetu angaliweza kuinua na kuonyesha Rozari yake akasema
kwa makini na moyo wote: “Angalieni hazina yangu kubwa ya nyumba
yangu.” Naye baba Mtakatifu
Yohani Paulo wa II, kwa kuona
umuhimu wa Rozari Takatifu aliongeza mafumbo matano ya Mwanga.
Mama Bikira Maria amekuwa akitokea katika matukio
mbalimbali duniani, lakini kubwa na yenye msisitizo ni yale matokeo ya
Fatina 1917. Katika
Tokeo la sita na la mwisho kule Fatima,
13/10/1917 B. Maria alisema “Watu waendelee kusali Rozari kila siku”
; Hivyo sharti
tusali Rozari.
(b) Muundo wa Rozari
Takatifu.
i.
Kanuni ya Imani“Nasadiki
kwa Mungu…….
Rejea Siri ya
Rozari uk. 55-56 Biblia heb 11:6
ii.
Baba yetu“Sala
ya Bwana”
Ni sala
aliyofundisha Mungu.
Rejea Siri ya
Rozari- uk. 57-72
Rejea Biblia -
Mt.6:9-13
iii.
Salamu Maria“Maamkio
ya Malaika
Rejea Siri ya Rozari uk. 72-85
Biblia- Lk 1:28, Lk
1:42
iv.
Atukuzwe Baba………
Kuutukuza Utatu
Mtakatifu.
v.
Ee Yesu Mwema……..
Sala aliyotoa B.
Maria Fatima 13/7/1917 kuomba kwa Yesu
atuepushe na moto wa Jehanamu.
(a) Matendo ya
Furaha.(
J.tatu na J.mosi)
1.Maria
anapashwa habari na Malaika. ( Lk.1:28)
2.Maria alipoenda kumtembelea Elizabeti. (
Lk. 1:41-42 )
3.Yesu anazaliwa Betlehemu. (
Lk.2:7 )
4.Yesu anatolewa hekaluni. (
Lk. 2:22-23 )
5.Maria
anamkuta Yesu hekaluni. ( Lk. 2:46 )
(b)
Matendo ya uchungu.(J.nne
na Ijumaa )
1.Yesu anatoka jasho la damu. (
Lk. 22:44-45 )
2Yesu anapigwa mijeledi. (
Yn. 19:1 )
3.Yesu anavikwa taji la miiba kichwani. (
Mt. 27:28-29 )
4.Yesu anachukua msalaba. (
Yn. 19: 17 )
5.Yesu anakufa msalabani. (
Lk. 23: 46 )
( c )Matendo ya utukufu. ( J.tano
na J.pili )
1.Yesu anafufuka.
(
Mk. 16: 6 )
2.Yesu
anapaa mbinguni. ( Mdo. 1:9-11 )
3.Roho
Mt. anawashukia mitume. ( Mdo 2:2- 4 )
4.B.Maria anapalizwa mbinguni.
(
1 The 4:14-17 )
5.Maria
anawekwa malkia mbinguni. ( Ufu. 12:1 )
( d ) Matendo ya Mwanga. ( Alhamisi )
1.Yesu
anabatizwa mtoni Yordani. ( Mt. 3:16-17 )
2.Yesu
anageuza maji kuwa divai huko Kana. ( Yn. 2:3-5 )
3.Yesu
anatangaza ufalme wa Mungu. ( Mk. 1:14-15 )
4.Yesu
anageuka sura. ( Mt. 17: 1- 2 )
5.Yesu
anaweka Ekaristi Takatifu. ( Lk.22; 19- 20 )
Kusali Rozari
ni kutafakari Maisha,Mateso, kifo na utukufu wa Mkombozi wetu Yesu Kristu.
Yote haya yapo kwenye
Biblia Takatifu.
Rozari siyo mkusanyiko
wa Baba yetu na Salamu Maria nyingi ila ni muhtasari
Mtakatifu wa mafumbo ya maisha,
mateso kifo na utukufu wa Yesu na Maria.
Msomi Kajetani anasema……
kuacha kusali sala ya Baba yetu na salamu Maria ni kudondoka katika chambo
cha ndoto za shetani.
Sala hizi ni kinga nguvu na usalama
wa mioyo yetu.
B. Maria alimweleza Mt.
Getruda Hapajatokea
binadamu yeyote aliyeweza kumtungia kitu chochote kilicho kizuri kama “Salamu
Maria
“Hapatakuwepo na maamkia yoyote yenye thamani katika
moyo wangu kama uzuri na heshima iliyopo
katika maneno hayo yaliyotoka kwa Mungu Baba.”
Rozari ina sehemu kuu mbili:-
(a)
Tafakari
(b)
Kusema kwa Sauti
Rejea –Siri ya Rozari uk. 22.
Rejea- Siri ya Rozari uk. 97
Comments
Post a Comment